IJUE ILANI YA CCM NGUZO ZA MAENDELEO YA TAIFA
10 Sep, 2025
40 Machapisho
Katika sekta ya nishati na miundombinu, Ilani ya CCM inalenga kupeleka umeme vijijini, kujenga barabara, madaraja, reli na bandari, Hatua hizi ni injini ya ukuaji wa uchumi na zinaunganisha wananchi wote bila kubagua.
Kwa upande wa afya, kipaumbele kimewekwa katika kuimarisha huduma za msingi, kujenga vituo vya afya, hospitali za kisasa na nyumba za watumishi, Lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania, popote alipo, anapata huduma bora na za haraka ili kulinda afya ya jamii na kuongeza nguvu kazi ya taifa.
Katika usafirishaji, Ilani imejipanga kuongeza uwekezaji kwenye barabara kuu, stendi za kisasa, reli ya kisasa (SGR) pamoja na mabasi yaendayo haraka, Hatua hizi zitapunguza gharama za safari, kuongeza ufanisi wa biashara, kurahisisha safari za wananchi na kufungua fursa za kibiashara mikoa yote nchini.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatikiFyuchaBilaStresi
#NchiImetuliaHatunaDeniNaSamia
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.