IJUE ILANI YA CCM NGUZO ZA MAENDELEO YA TAIFA
10 Sep, 2025
96 Machapisho
Katika sekta ya nishati na miundombinu, Ilani ya CCM inalenga kupeleka umeme vijijini, kujenga barabara, madaraja, reli na bandari, Hatua hizi ni injini ya ukuaji wa uchumi na zinaunganisha wananchi wote bila kubagua.
Kwa upande wa afya, kipaumbele kimewekwa katika kuimarisha huduma za msingi, kujenga vituo vya afya, hospitali za kisasa na nyumba za watumishi, Lengo ni kuhakikisha kila Mtanzania, popote alipo, anapata huduma bora na za haraka ili kulinda afya ya jamii na kuongeza nguvu kazi ya taifa.
Katika usafirishaji, Ilani imejipanga kuongeza uwekezaji kwenye barabara kuu, stendi za kisasa, reli ya kisasa (SGR) pamoja na mabasi yaendayo haraka, Hatua hizi zitapunguza gharama za safari, kuongeza ufanisi wa biashara, kurahisisha safari za wananchi na kufungua fursa za kibiashara mikoa yote nchini.
#KaziNaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatikiFyuchaBilaStresi
#NchiImetuliaHatunaDeniNaSamia
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo