SOMBI ASHIRIKI KAMPENI NZEGA MJINI,
22 Sep, 2025
99 Machapisho
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Rehema Sombi Omary (MNEC),ameshiriki Kampeni na kumuombea Kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan, na wagombea Ubunge Jimbo la Bukene, Nzega Vijijini na Nzega Mjini pamoja na kuwaonbea kura wagombea Udiwani wa CCM.
Ndugu Rehema Sombi amewaombea kura wagombea hao wa CCM katika Uzinduzi wa Kampeni uliofanyika Nzega Mjini Mkoa wa Tabora Leo Septemba 21, 2025.
Katika Uzinduzi huo wamehudhuria maelfu ya Wananchi kutoka sehemu mbalimbali , viongozi na wanachama wa CCM huku Mratibu wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi CCM) kanda ya Kati na Katibu Mkuu mstaafu wa chama hicho, Dkt. Bashiru Ali, akiwa Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Nzega Mjini .
Kwa upande mwingine Komredi Sombi amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili wagombea hao wapate kura nyingi za kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025. Amesisitiza Umoja na Mshikamano miongoni mwa wananchi huku akisema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndio Chama pekee ambacho kinashughulika na kutatua changamato za wananchi kwani kupitia ilani ya 2025 - 2030 imeainisha vipaumbele ambavyo kupitia wagombea hao wananchi watapata miradi Mingi ya Maendeleo Kwani ni ilani bora na inapimika.
#oktobatunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#fyuchabilaStresi
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo