SOMBI ASHIRIKI KAMPENI NZEGA MJINI,
22 Sep, 2025
56 Machapisho
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Ndugu Rehema Sombi Omary (MNEC),ameshiriki Kampeni na kumuombea Kura Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan, na wagombea Ubunge Jimbo la Bukene, Nzega Vijijini na Nzega Mjini pamoja na kuwaonbea kura wagombea Udiwani wa CCM.
Ndugu Rehema Sombi amewaombea kura wagombea hao wa CCM katika Uzinduzi wa Kampeni uliofanyika Nzega Mjini Mkoa wa Tabora Leo Septemba 21, 2025.
Katika Uzinduzi huo wamehudhuria maelfu ya Wananchi kutoka sehemu mbalimbali , viongozi na wanachama wa CCM huku Mratibu wa kampeni za Chama Cha Mapinduzi CCM) kanda ya Kati na Katibu Mkuu mstaafu wa chama hicho, Dkt. Bashiru Ali, akiwa Mgeni Rasmi katika Uzinduzi wa Kampeni Jimbo la Nzega Mjini .
Kwa upande mwingine Komredi Sombi amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili wagombea hao wapate kura nyingi za kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025. Amesisitiza Umoja na Mshikamano miongoni mwa wananchi huku akisema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndio Chama pekee ambacho kinashughulika na kutatua changamato za wananchi kwani kupitia ilani ya 2025 - 2030 imeainisha vipaumbele ambavyo kupitia wagombea hao wananchi watapata miradi Mingi ya Maendeleo Kwani ni ilani bora na inapimika.
#oktobatunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#fyuchabilaStresi
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.