SOMBI ATETA NA VIJANA WA KAHAMA AWATAKA KUWA MSTARI WA MBELE KUZISAKA KURA ZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN.
22 Sep, 2025
64 Machapisho
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Ndugu Rehema Sombi amekutana na Vijana UVCCM Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga Jana Septemba 20, 2025 katika Ofisi za CCM Wilaya huku akiteta nao kuhusu wajibu wao wa kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu Pamoja na kuhamasisha wengine wajitokeze kwa wingi kupiga kura.
Aidha amewaomba Vijana kuwa mstari wa mbele kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuhakikisha wagombea wote wa CCM ikiwemo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, wagombea Ubunge pamoja madiwani wanaibuka kidedea kwa kura nyingi za kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025. Pia ameelezea jinsi Ilani ya 2025-2030 ilivyobeba agenda ya Maendeleo kwa wananchi hivyo Vijana ni wajibu wao kuwahamasisha wananchi kupiga kura ili Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiendelee kushika Dola na kuendelea kuleta maendeleo kwa wananchi.
#tunazimazotetunawashakijani
#OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo