SOMBI ATETA NA VIJANA WA KAHAMA AWATAKA KUWA MSTARI WA MBELE KUZISAKA KURA ZA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN.
22 Sep, 2025
24 Machapisho
Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa na Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Ndugu Rehema Sombi amekutana na Vijana UVCCM Wilaya ya Kahama Mkoa wa Shinyanga Jana Septemba 20, 2025 katika Ofisi za CCM Wilaya huku akiteta nao kuhusu wajibu wao wa kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu Pamoja na kuhamasisha wengine wajitokeze kwa wingi kupiga kura.
Aidha amewaomba Vijana kuwa mstari wa mbele kujitokeza kwa wingi kupiga kura ili kuhakikisha wagombea wote wa CCM ikiwemo Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, wagombea Ubunge pamoja madiwani wanaibuka kidedea kwa kura nyingi za kishindo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29,2025. Pia ameelezea jinsi Ilani ya 2025-2030 ilivyobeba agenda ya Maendeleo kwa wananchi hivyo Vijana ni wajibu wao kuwahamasisha wananchi kupiga kura ili Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiendelee kushika Dola na kuendelea kuleta maendeleo kwa wananchi.
#tunazimazotetunawashakijani
#OktobatunatikiFyuchaBilaStresi
#TunazimaZoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.