SAMIA SCHOLARSHIP NI UFADHILI WA BURE KABISA SIO MKOPO
24 Sep, 2025
78 Machapisho
Kibaha, pwani.
23/09/2025
Mkuu wa idara ya uhusiano wa Kimataifa vyuo na vyuo Vikuu UVCCM Taifa Ndg Emanuel Martine* leo tarehe 23.09.2025 akiambatana na Mwenyekiti wa UVCCM vyuo na vyuo Vikuu mkoa wa pwani Ndg Mwanaidi Khamis Ramadhani amefanya mazungumzo na waalimu na wanafunzi wa shule ya Sekondari kibaha ambapo alipita kuwapa salamu za upendo za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM Dkt Samia Suluhu Hassan.
Ndg Martine ametumia fursa hiyo kuwaambia wanafunzi wa kidato cha tano na cha sita kuwa Dkt Samia Suluhu Hassan anawapenda wanafunzi na wazazi na walezi wa wanafunzi kwani ameanzisha mifuko ya ufadhili wa bure katika masomo ya sayansi, mifuko hiyo ni
1. SAMIA SCHOLARSHIP- huu ni ufadhili wa asilimia mia kwa wanafunzi waliofanya vizuri zaidi katika masomo ya sayansi, huu sio mkopo wa chuo ni ufadhili wa bure kabisa.
2. â SAMIA EXTENDED PROGRAM- huu ni ufadhili wa kusoma nje ya nchi katika vyuo vya umahiri Duniani katika mambo ya Data sayansi na akili unde
3. â SAMIA INNOVATION FUNDS
Pia Dkt Samia ameongeza bajeti ya Bodi ya mikopo ili wanafunzi wanaomaliza kidato cha sita waweze kupata mikopo ya chuo
Awali kabla ya kupita shule ya sekondari kibaha Ndg Emanuel Martine alipata wasaa wa kuzungumza na Viongozi wa UVCCM vyuo na vyuo Vikuu mkoa wa pwani wakiongozwa na Ndg Mwanaidi khamis Ramadhani pamoja na timu ya ushindi ya vyuo na vyuo vikuu mkoa wa pwani na kuwataka kuendelea kutafuta kura za CCM.
Ndg Emanuel Martine amewasisitiza wanavyuo kuzitafuta kura za Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan mtu kwa mtu, simu kwa simu, mitaa kwa mitaa, nyumba kwa nyumba, vijiwe kwa Vijiwe na makundi kwa makundi ili kuhakikisha Kura za Dkt Samia Suluhu Hassan zinapatikana kwa wingi, Samia ashinde kwa kushindo (fact and figure)
Kwa upande wao, Wanavyuo wamekikubali Chama Cha Mapinduzi Kwa Kuwa kimewawekea Sera bora Kwa Wanavyuo Kupitia Ilani yake 2025/30 Iliyoelekeza Ongezeko la Wanufaika wa Mikopo ya Elimu ya Juu pamoja na Uboreshwaji Mitaala ya Elimu utakaosaidia katika Kuongeza mianya ya Ajira na kujiajiri mara baada ya Kuhitimu CCM inawapenda wanavyuo wote wa vyuo vya kati na vyuo Vikuu
#OktobaTunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazaZoteTunawashaKijani
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo