SOMBI AZINDUA RASMI KAMPENI JIMBO LA DIMANI
24 Sep, 2025
30 Machapisho
Dimani – Zanzibar, 23 Septemba 2025:
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndugu Rehema Sombi Omary (MNEC), leo amezindua rasmi kampeni za CCM katika Jimbo la Dimani, Zanzibar.
Akizungumza na wananchi na wanachama waliojitokeza kwa wingi katika mkutano wa hadhara, Ndugu Rehema alisema kuwa CCM ndicho chama pekee kinachoweza kuwaletea wananchi maendeleo ya kweli na kuendelea kulinda maslahi ya Taifa.
MAFANIKIO YA ILANI YA 2020–2030 ZANZIBAR
Katika hotuba yake, alieleza kuwa kupitia Ilani ya CCM 2020–2030, Serikali ya Awamu ya Nane inayoongozwa na Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi imefanikisha miradi mikubwa ya maendeleo ikiwemo:
- Ujenzi wa shule mpya za kisasa.
- Vituo vya afya vilivyo karibu na wananchi.
- Masoko yenye hadhi ya kimataifa.
- Barabara za lami zinazounganisha mjini na vijijini
Katika kampeni hizo, Ndugu Rehema aliwanadi wagombea wa CCM kwa Jimbo la Dimani:
- Ndugu Nabil Ahmed Abdillah – Mgombea Ubunge.
- Ndugu Mwanaasha Khamis Juma – Mgombea Uwakilishi.
- Wagombea Udiwani wa kata mbili za Dimani."
WITO KWA WANANCHI
Aidha, aliwaombea wananchi wa Dimani kura kwa wagombea wote wa CCM, akisisitiza umuhimu wa kumchagua Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Mgombea Urais wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025.
Ndugu Rehema pia aliwataka wananchi kudumisha amani, mshikamano na utulivu katika kipindi chote cha uchaguzi.
#SautiYenu
#OktobaTunatiki
#fyuchabilastres
#KaziNaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.