Rais Dkt. Mwinyi Apokea Pole Kufuatia Kifo cha Kaka Yake
26 Sep, 2025
53 Machapisho
Zanzibar, 26 Septemba 2025 – Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amepokea salamu za pole kufuatia kifo cha kaka yake mpendwa, Marehemu Abbas Ali Mwinyi, kilichotokea jana tarehe 25 Septemba 2025.
Katika kuonesha mshikamano wa kitaifa na upendo wa kidugu, viongozi mbalimbali wa ngazi za juu walifika nyumbani kwa familia ya marehemu huko Bweleo, Mkoa wa Mjini Magharibi, kutoa mkono wa pole na rambirambi.
Uongozi wa Kitaifa Wajumuika
Miongoni mwa viongozi walioungana na Rais Mwinyi ni:
- Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan
- Naibu Waziri Mkuu, Mhe. Dotto Mashaka Biteko
- Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu
- Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla
- Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zuberi Ali Maulid
- Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro
- pamoja na viongozi wengine mbalimbali wa Serikali, chama na taasisi za dini.
RATIBA YA MAZISHI
Kwa mujibu wa familia, Marehemu Abbas Ali Mwinyi atasaliwa katika Masjid Jamia Zinjibar, Mazizini mara baada ya Sala ya Ijumaa, kisha kuzikwa Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, leo tarehe 26 Septemba 2025.
Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina.
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo