πππ₯π¦π§ π§ππ π π©π’π§ππ₯π¦ πππ§ππ©π πͺππ£π’ π§ππ¬ππ₯π ππ¨π§πππ π’ππ§π’ππ ππͺπ πππ§. π¦ππ ππ
28 Sep, 2025
32 Machapisho
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM Taifa na pia Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM kutoka Mkoa wa Katavi, Eng. Debora Joseph Tluway, amekutana na vijana wapiga kura wapya walioshiriki kongamano la mbio za Mwenge lililofanyika katika Halmashauri ya Mpimbwe, Mkoa wa Katavi.
Katika kongamano hilo, Eng. Debora aliwapatia vijana elimu kuhusu mchakato wa upigaji kura, huku akisisitiza umuhimu wa kuchagua viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kama nguzo ya maendeleo ya Taifa. Alisisitiza kuwa kura ya vijana ndiyo nguzo ya kulinda amani, mshikamano, na maendeleo endelevu yaliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Washiriki wa kongamano hilo walionesha shukrani zao kwa Serikali ya Dkt. Samia kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa katika sekta ya elimu wilayani humo. Walibainisha kuwa ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa pamoja na elimu bila malipo hadi kidato cha sita ni neema kubwa kwa watoto wa Kitanzania na kielelezo cha uongozi wenye kujali maisha ya wananchi.
Aidha, vijana hao wapiga kura wapya waliapa kwa sauti moja kuwa ifikapo 29 Oktoba 2025 watamtikia kura ya NDIO Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sambamba na wagombea wote wa CCM katika ngazi zote, wakisisitiza kuwa maendeleo yanayoonekana sasa ni sababu ya kuipa CCM ushindi wa kishindo
#OktobaTunatikiβ
β
β
#FyuchaBilaStresi
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.