ð—™ð—œð—¥ð—¦ð—§ ð—§ð—œð— ð—˜ ð—©ð—¢ð—§ð—˜ð—¥ð—¦ ð—žð—”ð—§ð—”ð—©ð—œ ð—ªð—”ð—£ð—¢ ð—§ð—”ð—¬ð—”ð—¥ð—œ ð—žð—¨ð—§ð—œð—žð—œ ð—¢ð—žð—§ð—¢ð—•ð—” ð—žð—ªð—” ð——ð—žð—§. ð—¦ð—”ð— ð—œð—”
28 Sep, 2025
80 Machapisho
Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM Taifa na pia Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM kutoka Mkoa wa Katavi, Eng. Debora Joseph Tluway, amekutana na vijana wapiga kura wapya walioshiriki kongamano la mbio za Mwenge lililofanyika katika Halmashauri ya Mpimbwe, Mkoa wa Katavi.
Katika kongamano hilo, Eng. Debora aliwapatia vijana elimu kuhusu mchakato wa upigaji kura, huku akisisitiza umuhimu wa kuchagua viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kama nguzo ya maendeleo ya Taifa. Alisisitiza kuwa kura ya vijana ndiyo nguzo ya kulinda amani, mshikamano, na maendeleo endelevu yaliyoasisiwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Washiriki wa kongamano hilo walionesha shukrani zao kwa Serikali ya Dkt. Samia kutokana na mageuzi makubwa yaliyofanywa katika sekta ya elimu wilayani humo. Walibainisha kuwa ujenzi wa vyumba vipya vya madarasa pamoja na elimu bila malipo hadi kidato cha sita ni neema kubwa kwa watoto wa Kitanzania na kielelezo cha uongozi wenye kujali maisha ya wananchi.
Aidha, vijana hao wapiga kura wapya waliapa kwa sauti moja kuwa ifikapo 29 Oktoba 2025 watamtikia kura ya NDIO Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sambamba na wagombea wote wa CCM katika ngazi zote, wakisisitiza kuwa maendeleo yanayoonekana sasa ni sababu ya kuipa CCM ushindi wa kishindo
#OktobaTunatiki✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko