MWAKITINYA, MWANRI MGUU KWA MGUU MITAANI KUZISAKA KURA ZA DKT. SAMIA
28 Sep, 2025
62 Machapisho
Kahama, Shinyanga
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Tanzania Bara, Ndg. Mussa Peter Mwakitinya , leo 28 Septemba 2025 ameungana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa mstaafu wa Tabora, Ndg. Aggrey Mwanri, katika harakati za kusaka kura za kishindo kwa ajili ya Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Katika matembezi na mikutano ya mitaani, viongozi hao waliungana na wananchi wa Kahama na kuwasisitizia umuhimu wa kuendelea kuipa CCM ridhaa ya kuongoza nchi, wakibainisha kuwa utekelezaji wa Ilani ya CCM umeleta matokeo chanya yanayoonekana kwa macho ya kila Mtanzania.
Wananchi wa Kahama kwa upande wao walionesha kuridhishwa na maendeleo makubwa yaliyoletwa na Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Dkt. Samia. Wameahidi kwamba ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, watamtikia kura ya NDIO kwa kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wote wa CCM kuanzia ngazi ya ubunge hadi udiwani.
#OktobaTunatikiā
#TunazimaZoteTunawashaKijani
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.