MWAKITINYA, MWANRI MGUU KWA MGUU MITAANI KUZISAKA KURA ZA DKT. SAMIA
28 Sep, 2025
120 Machapisho
Kahama, Shinyanga
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Naibu Katibu Mkuu wa UVCCM Tanzania Bara, Ndg. Mussa Peter Mwakitinya , leo 28 Septemba 2025 ameungana na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa mstaafu wa Tabora, Ndg. Aggrey Mwanri, katika harakati za kusaka kura za kishindo kwa ajili ya Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Katika matembezi na mikutano ya mitaani, viongozi hao waliungana na wananchi wa Kahama na kuwasisitizia umuhimu wa kuendelea kuipa CCM ridhaa ya kuongoza nchi, wakibainisha kuwa utekelezaji wa Ilani ya CCM umeleta matokeo chanya yanayoonekana kwa macho ya kila Mtanzania.
Wananchi wa Kahama kwa upande wao walionesha kuridhishwa na maendeleo makubwa yaliyoletwa na Serikali ya CCM chini ya uongozi wa Dkt. Samia. Wameahidi kwamba ifikapo tarehe 29 Oktoba 2025, watamtikia kura ya NDIO kwa kishindo Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na wagombea wote wa CCM kuanzia ngazi ya ubunge hadi udiwani.
#OktobaTunatiki✅
#TunazimaZoteTunawashaKijani
#KazinaUtuTunasongaMbele
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko