SAMIA EXTENDED PROGRAM: WANAFUNZI KUTAFUTIWA VYUO VYA UMAHIRI DUNIANI KWA UFADHILI WA DKT. SAMIA
29 Sep, 2025
27 Machapisho
Mbeya, 29 Septemba 2025
Katika mwendelezo wa ziara zake za kukutana na makundi mbalimbali ya vijana na wanavyuo, Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa Vyuo na Vyuo Vikuu UVCCM Taifa Ndg. Emanuel Martine leo amekutana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Loleza, Mkoa wa Mbeya.
Akiwa mbele ya wanafunzi hao, Ndg. Martine amewataka kuongeza bidii katika masomo ili kujiweka kwenye nafasi ya kunufaika na mpango kabambe wa SAMIA EXTENDED PROGRAM. Kupitia mpango huu, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan itawatafutia wanafunzi wenye ufaulu bora nafasi za masomo katika vyuo vikuu vya umahiri duniani kwa ufadhili kamili wa serikali.
Aidha, Martine alisisitiza kuwa Dkt. Samia ni Kiongozi mwenye moyo wa kipekee, kiongozi anayegusa maisha ya kila kijana na kila Mtanzania. Ni kiongozi anayeweka elimu, ustawi na maendeleo ya vijana mbele kama injini kuu ya kulijenga Taifa bora lenye matumaini na maendeleo endelevu
#OktobaTunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazoZoteTunawashaKijani
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.