SAMIA EXTENDED PROGRAM: WANAFUNZI KUTAFUTIWA VYUO VYA UMAHIRI DUNIANI KWA UFADHILI WA DKT. SAMIA
29 Sep, 2025
72 Machapisho
Mbeya, 29 Septemba 2025
Katika mwendelezo wa ziara zake za kukutana na makundi mbalimbali ya vijana na wanavyuo, Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa Vyuo na Vyuo Vikuu UVCCM Taifa Ndg. Emanuel Martine leo amekutana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Loleza, Mkoa wa Mbeya.
Akiwa mbele ya wanafunzi hao, Ndg. Martine amewataka kuongeza bidii katika masomo ili kujiweka kwenye nafasi ya kunufaika na mpango kabambe wa SAMIA EXTENDED PROGRAM. Kupitia mpango huu, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan itawatafutia wanafunzi wenye ufaulu bora nafasi za masomo katika vyuo vikuu vya umahiri duniani kwa ufadhili kamili wa serikali.
Aidha, Martine alisisitiza kuwa Dkt. Samia ni Kiongozi mwenye moyo wa kipekee, kiongozi anayegusa maisha ya kila kijana na kila Mtanzania. Ni kiongozi anayeweka elimu, ustawi na maendeleo ya vijana mbele kama injini kuu ya kulijenga Taifa bora lenye matumaini na maendeleo endelevu
#OktobaTunatiki✅✅
#KazinaUtuTunasongaMbele
#TunazoZoteTunawashaKijani
#WanavyuoChaguaCCMChaguaSAMIA
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko