🗓ï¸BILA CCM MADHUBUTI NCHI YETU ITAYUMBA
10 Oct, 2025
62 Machapisho
📠Tarehe 10/10/2025
â°Butiama-Mara
Akiwa katika mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika leo Butiama Mkoani Mara, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza kwa msisitizo mkubwa kuwa uimara wa Taifa letu unategemea Uimara wa CCM.
Amesema chama hiki kimekuwa nguzo kuu ya amani, umoja na maendeleo tangu kupatikana kwa uhuru, na bila misingi imara ya CCM, nchi inaweza kuyumba kisiasa na kiuchumi Dkt. Samia amewataka Watanzania wote kuendelea kukiamini na kukiunga Mkono CCM kwa vitendo, hasa kwa kujitokeza kwa wingi tarehe 29 Oktoba kumpigia kura ili kuendeleza safari ya maendeleo yenye Uthabiti, Utulivu na Matumaini Kwa Wote.
#OktobaTunatiki
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo