Dkt. Hussein Ali Mwinyi asema atayatekeleza Mambo Matatu Muhimu Kwa Vijana
10 Oct, 2025
55 Machapisho
Kusini Unguja, Zanzibar – Mgombea nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameyataja mambo matatu ambayo atayatekeleza kwa vijana endapo atachaguliwa katika uongozi ujao.
Kauli hiyo ameitoa wakati akizungumza na vijana wa vyuo vikuu na makundi mbalimbali katika Chuo cha Mafunzo ya Vijana Tunguu, kilichopo Wilaya ya Kusini Unguja, mkoa wa Kusini Unguja.
Dk. Mwinyi amesema kuwa vijana wanahitaji fursa katika maeneo matatu muhimu: elimu, ajira na nafasi za uongozi.
"Tulipoingia tulikuta bajeti ya elimu ni shilingi bilioni 80 tu, sasa tumeongeza hadi shilingi bilioni 864, hivyo kipaumbele cha kwanza ni elimu ili vijana wetu waelimike. Kwa upande wa ajira, tumeahidi kutoa nafasi za ajira 350,000, na safari hii tutaongeza idadi hiyo zaidi kwa ajili ya vijana. Na fursa ya tatu ambayo vijana wanahitaji ni nafasi za uongozi, ambapo tutatoa nafasi za vijana katika uongozi wa serikali," alisema Dk. Hussein Ali Mwinyi.
Vijana waliohudhuria mkutano huo wameshuhudia kauli hizi kwa furaha kubwa, wakionyesha hamasa ya kushirikiana na Dk. Mwinyi kuhakikisha kwamba vijana wanapata fursa na ushiriki mkubwa katika maendeleo ya Zanzibar.
#KazinaUtuTunasongaMbele
#OktobaTunatiki
#TokaNitokeTukatiki
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo