RAIS MWINYI AISHUKURU SERIKALI YA OMAN KWA KUENDELEZA USHIRIKIANO NA ZANZIBAR
10 Oct, 2025
6 Machapisho
Zanzibar, 09 Oktoba 2025
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ameishukuru Serikali ya Oman na kupongeza uhusiano mwema wa kindugu na kihistoria uliopo kati ya Zanzibar na Oman.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo tarehe 09, Oktoba 2025, alipokutana na Waziri wa Mambo ya Kale na Utalii wa Oman, Mheshimiwa Sheikh Salim bin Mohammed Al Mahrouqi, aliyefuatana na Balozi Mdogo wa Oman anayefanya kazi zake Zanzibar, Mheshimiwa Said Salim Al Sinawi, pamoja na ujumbe kutoka Wizara hiyo ya Oman.
Katika mazungumzo hayo, Rais Dkt. Mwinyi amesisitiza dhamira ya Serikali ya Zanzibar kuendeleza uhusiano huo wa kihistoria kwa manufaa ya pande zote mbili, hususan katika maeneo ya utalii, utamaduni na uhifadhi wa urithi wa kihistoria.
Kwa upande wake, Waziri Mahrouqi amemshukuru Rais Dkt. Mwinyi kwa ukarimu wake na kueleza dhamira ya Serikali ya Oman kuendeleza ushirikiano uliopo, hususan katika programu ya ukarabati wa majengo ya kihistoria yanayofadhiliwa na Oman.
Akiwa Zanzibar, Waziri Mahrouqi, akiwa na mwenyeji wake Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar, Mheshimiwa Mudrick Ramadhan Soraga, ametembelea majengo mbalimbali yanayofadhiliwa na Serikali ya Oman, yakiwemo Beit al Ajaib, Mtoni Palace, Kibweni Palace pamoja na majengo mengine yaliyomo ndani ya Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.