Banda la UVCCM Linaendelea Viwanja vya Uhindini
14 Oct, 2025
60 Machapisho
UVCCM imeendelea kutoa elimu kwa vijana katika viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya, katika maonesho ya Wiki ya Vijana kitaifa yanayoendelea. UVCCM imeendelea kuelimisha vijana namna sahihi ya kupiga kura za Mgombea wa Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutumia mfano wa karatasi ya kura, pamoja na umuhimu wa kushiriki uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, na kuchagua wabunge na madiwani wa CCM.
Vijana pia wameendelea kupewa elimu ya amani na utulivu wa Taifa, umuhimu wa uzalendo na jinsi ya kutumia haki zao za kidemokrasia kwa njia salama kupiga kura. Huduma zingine ni pamoja na usajili wa kielektroniki wa wanachama wa CCM, urejeshaji wa namba za kielektroniki kwa waliopoteza, na elimu ya mfumo wa Kijani Ilani Chatbot (Ilani ya CCM kidijitali kwa vijana). Huduma hizi zimevutia vijana wengi kuja kujifunza na kushiriki katika banda la UVCCM.
KAULI MBIU: NGUVU KAZI YA VIJANA KWA MAENDELEO ENDELEVU 💪🇹🇿
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#TokaNitokeTukatiki ✅
#OktobaTunatiki ✅
#TunazimazoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo