Banda la UVCCM Linaendelea Viwanja vya Uhindini
14 Oct, 2025
11 Machapisho
UVCCM imeendelea kutoa elimu kwa vijana katika viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya, katika maonesho ya Wiki ya Vijana kitaifa yanayoendelea. UVCCM imeendelea kuelimisha vijana namna sahihi ya kupiga kura za Mgombea wa Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutumia mfano wa karatasi ya kura, pamoja na umuhimu wa kushiriki uchaguzi wa Oktoba 29, 2025, na kuchagua wabunge na madiwani wa CCM.
Vijana pia wameendelea kupewa elimu ya amani na utulivu wa Taifa, umuhimu wa uzalendo na jinsi ya kutumia haki zao za kidemokrasia kwa njia salama kupiga kura. Huduma zingine ni pamoja na usajili wa kielektroniki wa wanachama wa CCM, urejeshaji wa namba za kielektroniki kwa waliopoteza, na elimu ya mfumo wa Kijani Ilani Chatbot (Ilani ya CCM kidijitali kwa vijana). Huduma hizi zimevutia vijana wengi kuja kujifunza na kushiriki katika banda la UVCCM.
KAULI MBIU: NGUVU KAZI YA VIJANA KWA MAENDELEO ENDELEVU 💪🇹🇿
#KazinaUtuTunasongaMbele ✅
#TokaNitokeTukatiki ✅
#OktobaTunatiki ✅
#TunazimazoteTunawashaKijani
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.