SERIKALI YA CCM KUJENGA TAWI LA JKCI GEITA MJINI
🗓 13 Oktoba 2025
📠Geita Mjini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan akiinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi akiwa katika jimbo la Geita Mjini amewaeleza wananchi kuwa Serikali imejipanga kujenga tawi la JKCI ndani ya jimbo hilo ili kuwasogezea wananchi huduma ya matibabu ya moyo.
Hatua hii ni ushahidi tosha wa dira ya maendeleo ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kikwazo cha umbali wala gharama kubwa, Ujenzi wa tawi la JKCI Geita Mjini utakuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya afya ya mkoa huo, kwani utapunguza rufaa nyingi kwenda Dar es Salaam, kuongeza ajira kwa wataalamu wa afya na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kibingwa. Wananchi wa Geita sasa wanapaswa kuona hili kama ishara ya upendo wa kweli wa Serikali ya CCM kwao Serikali inayosikiliza, inayotekeleza, na inayoweka uhai wa wananchi wake mbele ya yote.
#OktobaTunatiki ✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KATIBU MKUU WA UVCCM KUONGOZA KIKAO CHA SEKRETARIETI YA BARAZA KUU LA UVCCM, ZANZIBAR
09 Feb, 2026
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Ndugu Halid Mwinyi (MNEC), anatarajiwa kuongoza kikao cha Sekretarieti ya Baraza Kuu la UVCCM kitakachofanyika Jumanne, tarehe 10 Februari 2026, katika Chuo cha Umoja wa Vijana Tunguu, Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA AAGIZA UTUNZAJI WA MIUNDOMBINU, UJENZI WA KITUO CHA WATOTO NA ELIMU YA ZIMAMOTO SOKO JIPYA LA KARIAKOO
08 Feb, 2026
Dar es Salaam 08 Februari 2026 Katika kulinda uwekezaji wa umma na kuhakikisha thamani ya fedha za wananchi inalindwa, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesisitiza umuhimu wa kutunza na kusimamia miundombinu ya Soko
RAIS DKT. SAMIA AZINDUA SOKO JIPYA LA KARIAKOO: AFUNGUA UKURASA MPYA WA TUMAINI LA KIUCHUMI, AAGIZA HAKI, UWAZI NA USALAMA KWA WAFANYABIASHARA
08 Feb, 2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Jengo Jipya la Soko la Kariakoo