SERIKALI YA CCM KUJENGA TAWI LA JKCI GEITA MJINI
🗓 13 Oktoba 2025
📍 Geita Mjini
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan akiinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi akiwa katika jimbo la Geita Mjini amewaeleza wananchi kuwa Serikali imejipanga kujenga tawi la JKCI ndani ya jimbo hilo ili kuwasogezea wananchi huduma ya matibabu ya moyo.
Hatua hii ni ushahidi tosha wa dira ya maendeleo ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kikwazo cha umbali wala gharama kubwa, Ujenzi wa tawi la JKCI Geita Mjini utakuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya afya ya mkoa huo, kwani utapunguza rufaa nyingi kwenda Dar es Salaam, kuongeza ajira kwa wataalamu wa afya na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kibingwa. Wananchi wa Geita sasa wanapaswa kuona hili kama ishara ya upendo wa kweli wa Serikali ya CCM kwao Serikali inayosikiliza, inayotekeleza, na inayoweka uhai wa wananchi wake mbele ya yote.
#OktobaTunatiki ✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki ✅
Habari Zinazohusiana
KURA YANGU SAUTI YANGU
26 Oct, 2025
Ni haki yangu kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba 29, 2025
KAWAIDA: "WATAKE WASITAKE CCM ITASHINDA KWA KISHINDO KIKUBWA TAREHE 29"
26 Oct, 2025
Mwenyekiti wa jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa komredi Mohammed Ali Kawaida akizungumza na wananchi walio jitokeza kwa wingi katika Ufungaji wa Kampeni Jimbo la Chaani Mkoa wa Kaskazini Unguja.
MARTINE AHAMASISHA WAPIGA KURA KUBEBA KADI ZAO OKTOBA 29 NA KUTIKI KWA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN
26 Oct, 2025
Dar es Salaam, Oktoba 25, 2025 Mkuu wa Idara ya Uhusiano wa Kimataifa wa Vyuo na Vyuo Vikuu Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Ndg. Emanuel Martine, amewahamasisha wafanyabiashara, wajasiriamali, wateja na wadau mbalimbali wa Soko la Mabibo jijini Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kupiga kura tarehe 29 Oktoba 2025, wakichagua kwa kishindo wagombea wote wa CCM.