UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

SERIKALI YA CCM KUJENGA TAWI LA JKCI GEITA MJINI

14 Oct, 2025 8 Machapisho

🗓 13 Oktoba 2025

📍 Geita Mjini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan akiinadi Ilani ya Chama cha Mapinduzi akiwa katika jimbo la Geita Mjini amewaeleza wananchi kuwa Serikali imejipanga kujenga tawi la JKCI ndani ya jimbo hilo ili kuwasogezea wananchi huduma ya matibabu ya moyo. 

Hatua hii ni ushahidi tosha wa dira ya maendeleo ya Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora za afya bila kikwazo cha umbali wala gharama kubwa, Ujenzi wa tawi la JKCI Geita Mjini utakuwa chachu ya mageuzi makubwa katika sekta ya afya ya mkoa huo, kwani utapunguza rufaa nyingi kwenda Dar es Salaam, kuongeza ajira kwa wataalamu wa afya na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia huduma za kibingwa. Wananchi wa Geita sasa wanapaswa kuona hili kama ishara ya upendo wa kweli wa Serikali ya CCM kwao Serikali inayosikiliza, inayotekeleza, na inayoweka uhai wa wananchi wake mbele ya yote.

#OktobaTunatiki ✅✅✅
#FyuchaBilaStresi
#TokaNitokeTukatiki ✅