UVCCM
Tafadhali subiri...
UMOJA WA VIJANA WA CCM (UVCCM)

Habari & Matukio

Habari za CCM, Habari za Vijana, Habari za Maendeleo n.k

AHSANTE KAGERA KWA MAPOKEZI MAZURI YA ILANI YA CCM
17 Oct, 2025
00:00

AHSANTE KAGERA KWA MAPOKEZI MAZURI YA ILANI YA CCM

Serikali ya Chama Cha Mapinduzi Chini ya Mwenyekiti wake Dkt Samia Suluhu Hassan ameendelea kuinadi ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera leo na kuahidi ahadi zifuatazo zilizopo kwenye ilani ya Chama Cha Mapinduzi ndani ya mkoa wa Kagera

Soma Zaidi
DKT SAMIA AWAPONGEZA VIJANA WA HAMASA
17 Oct, 2025
00:00

DKT SAMIA AWAPONGEZA VIJANA WA HAMASA

Mgombea wa kiti cha Urais kupitia tiketi ya CCM Dkt Samia Suluhu Hassan wakati akihitimisha Ziara yake Mkoani Kagera amefanya mkutano wa hadhara katika jimbo la Bukoba Mjini na kuwashukuru viongozi wa chama, wananchi vijana wa hamasa na makundi yote kwa ujumla kwa mapokezi na ushiriki wao mzuri wa mikutano yake ndani ya mkoa huo.

Soma Zaidi
DKT.MWINYI ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA BIASHARA ENEO LA DARAJANI
16 Oct, 2025
00:00

DKT.MWINYI ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA BIASHARA ENEO LA DARAJANI

Mgombea wa nafasi ya Rais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema lengo la Serikali ni kuendelea kuliimarisha eneo la Darajani na kujenga miundombinu zaidi ili wafanyabiashara wapate maeneo mazuri na ya kisasa ya kufanyia biashara.

Soma Zaidi
SERIKALI KUTOA NYENZO NA MITAJI KUWEZESHA UVUVI WA KISASA
16 Oct, 2025
00:00

SERIKALI KUTOA NYENZO NA MITAJI KUWEZESHA UVUVI WA KISASA

Dkt Samia Suluhu Hassan ambaye ni Mgombea wa kiti cha urais wa Jamhuri Ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi akiwa Wilaya Ya Bukoba Mkoani Kagera amesema kuwa wataimarisha Sekta ya Uvuvi kwa kwa kutoa Nyenzo mbalimbali zitakazosaidia kwenye uvuvi na kutoa mitaji kwa wavuvi.

Soma Zaidi
SERIKALI KUKAMILISHA TAWI LA CHUO KIKUU CHA UDSM KAGERA
16 Oct, 2025
00:00

SERIKALI KUKAMILISHA TAWI LA CHUO KIKUU CHA UDSM KAGERA

Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Ndugu Samia Suluhu Hassan akiwa Bukoba Mjini, Mkoa wa Kagera, amesema kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika elimu ya juu kwa kukamilisha tawi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Kagera hatua itakayokuza fursa za elimu, kuongeza utafiti na kuimarisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi katika Ukanda wa ziwa.

Soma Zaidi
SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KAGERA
16 Oct, 2025
00:00

SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA KAGERA

Akiwa Bukoba Mjini Mkoa wa Kagera, Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha dhamira thabiti ya kuendeleza uboreshaji wa miundombinu ya barabara ili kufungua fursa zaidi za kiuchumi, kurahisisha usafirishaji wa mazao na huduma, pamoja na kuunganisha vijiji na miji kupitia barabara za kisasa.

Soma Zaidi