MKUU WA MKOA WA SONGWE AFURAHISHWA NA UBUNIFU WA UVCCM KUPITIA MFUMO WA “KIJANI ILANI CHATBOT
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Mheshimiwa Jabiri Omari Makame, ametembelea banda la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) katika Maonesho ya Wiki ya Vijana Kitaifa yaliyotamatika katika Viwanja vya Uhindini Jijini Mbeya leo tarehe 14 Oktoba 2025 na kutoa pongezi kwa ubunifu wa kidijitali uliofanywa na vUVCCM chini ya uongozi bora wa Mwenyekiti wa UVCCM Taifa, Ndugu Mohamed Ali Kawaida (MCC).
Soma Zaidi
JESSICA MSHAMA AONGOZA MATEMBEZI YA HAMASA MULEBA
Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi wa UVCCM Taifa, Ndg. Jessica Mshama, ameongoza matembezi ya maelfu ya vijana wa hamasa wilayani Muleba, mkoani Kagera, leo tarehe 15 Oktoba 2025, kuelekea kwenye mkutano wa hadhara wa Mgombea wa Urais wa CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Soma Zaidi
MRADI WA MAJI WA ZIWA VIKTORIA KUWANUFAISHA WANAMULEBA
Ahadi za Dkt. Samia Suluhu Hassan zinaendelea kutafsiriwa kwa vitendo kupitia utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati inayogusa maisha ya wananchi moja kwa moja, ikiwemo mradi wa maji safi na salama kutoka Ziwa Viktoria unaoelekezwa hadi Wilaya ya Muleba.
Soma Zaidi
SERIKALI KUKAMILISHA UJENZI WA CHUO CHA VETA KYAKA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika Mkutano wa kampeni Uliofanyika Muleba, ameeleza dhamira ya Serikali kukamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Kyaka, hatua itakayowezesha vijana wa Kagera kupata mafunzo bora ya ufundi stadi na kujiajiri.
Soma Zaidi
SERIKALI CCM KULETA BOTI MBILI ZA KUSAFIRISHA WAGONJWA MULEBA
Katika kuimarisha huduma za afya kwa wananchi wanaoishi katika visiwa na Maeneo ya Mwambao wa Ziwa Victoria, Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametangaza mpango wa serikali wa kuleta boti mbili mpya za kisasa kwa ajili ya kusafirisha wagonjwa katika Halmashauri ya Muleba, Mkoa wa Kagera.
Soma Zaidi
DKT. SAMIA: TUMEMPOTEZA KIONGOZI MAHIRI NA MPENDA AMANI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mgombea Urais kupitia tiketi ya CCM Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya, Mheshimiwa Raila Amolo Odinga, akimtaja kuwa kiongozi mahiri, Mwanamajumui wa Afrika, mpenda amani na mtafuta suluhu.
Soma Zaidi